Mwanamke
106. Ukitaka kumjua mwanamke jua historia yake.
From → Falsafa za Enock Maregesi
Enock Maregesi is a Tanzanian author and winner of the Mabati-Cornell Kiswahili Prize for African Literature. His novel, KOLONIA SANTITA, was recognized for its excellent writing in African languages and its encouragement of translation from, between, and into African languages. In 2020, he was nominated for the Tällberg/Eliasson Global Leadership Prize and continues to live in Tanzania.
Kama unataka kuijua vizuri historia ya mwanamke hasa mwanamke unayetaka kuoana naye, usifanye naye mapenzi kwa miezi sita angalau. Ukifanya naye mapenzi kwa miezi sita au zaidi, au ndani ya miezi sita, halafu akakuchanganya kimapenzi, hutakuwa na uwezo mkubwa wa kuwasikiliza watu kuhusiana na historia yake.
Watu wakikuonyesha tabia zao za ndani kabisa usisubiri wakuonyeshe tena ndiyo uwaamini. Waamini kwa mara ya kwanza. Mtu, kwa mfano, akionyesha kwa mara ya kwanza kuwa si mwaminifu mwamini. Anajijua zaidi kuliko unavyomjua. Aidha, mtu akikwambia anakupenda halafu akakupiga ni mnafiki. Maneno yake yatasema anakupenda, vitendo vyake vitasema hakupendi. Ukiwa makini na matendo ya mtu, si maneno yake, utamjua. Sikiliza maoni ya watu! Kuwa makini na matendo ya mtu.
Mwaka mmoja na nusu unatosha kumjua mwanamke kabla ya ndoa. Miezi sita itakufanya ujue kama mwanamke anaweza kuwa mchumba. Mwaka mmoja na nusu utakufanya ujue kama mwanamke anaweza kuwa mke.
Finding the right person to love is something to take very seriously. Relationships don’t just work themselves out; you have to work on them. When you think you have found someone worth sharing the rest of your life with, you should do your homework before settling down.
Taking your time gives the best results.